Site uses cookies to provide basic functionality.

OK
LUKE
Prev Up Next Toggle notes
Chapter 17
Luke Swahili 17:1  Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.
Luke Swahili 17:2  Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.
Luke Swahili 17:3  Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, mwonye; akitubu, msamehe.
Luke Swahili 17:4  Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema Nimetubu, lazima umsamehe."
Luke Swahili 17:6  Naye Bwana akajibu, "Kama imani yenu ingekuwa ndogo hata kama chembe ndogo ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu: Ng'oka ukajipandikize baharini, nao ungewatii.
Luke Swahili 17:7  "Tuseme mmoja wenu ana mtumishi ambaye analima shambani au anachunga kondoo. Je, anaporudi kutoka shambani, atamwambia: Haraka, njoo ule chakula?
Luke Swahili 17:8  La! Atamwambia: Nitayarishie chakula, ujifunge tayari kunitumikia mpaka nitakapomaliza kula na kunywa, ndipo nawe ule na unywe.
Luke Swahili 17:9  Je utamshukuru huyo mtumishi kwa sababu ametimiza aliyoamriwa?
Luke Swahili 17:10  Hali kadhalika na ninyi mkisha fanya yote mliyoamriwa, semeni: Sisi ni watumishi tusio na faida, tumetimiza tu yale tuliyotakiwa kufanya."
Luke Swahili 17:11  Yesu akiwa safarini kwenda Yerusalemu alipitia mipakani mwa Samaria na Galilaya.
Luke Swahili 17:12  Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.
Luke Swahili 17:13  Wakapaza sauti wakisema, "Yesu Mwalimu, tuonee huruma!"
Luke Swahili 17:14  Alipowaona akawaambia, "Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani." Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.
Luke Swahili 17:15  Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.
Luke Swahili 17:16  Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.
Luke Swahili 17:17  Hapo Yesu akasema, "Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?
Luke Swahili 17:18  Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?"
Luke Swahili 17:19  Halafu akamwambia huyo mtu, "Simama, uende zako; imani yako imekuponya."
Luke Swahili 17:20  Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, "Ufalme wa Mungu utakuja lini?" Naye akawajibu, "Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.
Luke Swahili 17:21  Wala hakuna atakayeweza kusema, Uko hapa, au Uko pale. Kwa kweli Ufalme wa Mungu uko kati yenu."
Luke Swahili 17:22  Halafu akawaambia wanafunzi wake, "Siku zinakuja ambapo mtatamani kuona mojawapo ya siku za Mwana wa Mtu, lakini hamtaiona.
Luke Swahili 17:23  Na watu watawaambieni: Tazameni yuko hapa; ninyi msitoke wala msiwafuate.
Luke Swahili 17:24  Kwa maana kama vile umeme unavyotokea ghafla na kuangaza anga upande mmoja hadi mwingine, ndivyo Mwana wa Mtu atakavyokuwa siku yake.
Luke Swahili 17:25  Lakini kabla ya hayo, itambidi ateseke sana na kukataliwa na kizazi hiki.
Luke Swahili 17:26  Kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Mtu.
Luke Swahili 17:27  Watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka wakati ule Noa alipoingia katika safina. Gharika ikatokea na kuwaangamiza wote.
Luke Swahili 17:28  Itakuwa kama ilivyotokea wakati wa Loti. Watu waliendelea kula na kunywa, kununua na kuuza, kupanda mbegu na kujenga.
Luke Swahili 17:29  Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikanyesha kama mvua kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.
Luke Swahili 17:30  Ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mtu atakapofunuliwa.
Luke Swahili 17:31  "Siku hiyo, yeyote atakayekuwa juu ya paa asishuke nyumbani kuchukua mali yake. Kadhalika, naye atakayekuwa shambani asirudi nyuma.
Luke Swahili 17:33  Yeyote anayetaka kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na yeyote anayeipoteza, ataiokoa.
Luke Swahili 17:34  Nawaambieni, siku ile usiku watu wawili watakuwa wanalala pamoja, mmoja atachukuliwa na yule mwingine ataachwa.
Luke Swahili 17:35  Wanawake wawili watakuwa wakisaga nafaka pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa."
Luke Swahili 17:36  Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
Luke Swahili 17:37  Hapo wakamwuliza, "Ni wapi Bwana?" Naye akawaambia, "Ulipo mzoga, ndipo tai watakapokusanyikia."