Site uses cookies to provide basic functionality.

OK
LUKE
Prev Up Next Toggle notes
Chapter 4
Luke Swahili 4:1  Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
Luke Swahili 4:2  Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
Luke Swahili 4:3  Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
Luke Swahili 4:4  Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
Luke Swahili 4:5  Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
Luke Swahili 4:6  "Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
Luke Swahili 4:7  Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
Luke Swahili 4:8  Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
Luke Swahili 4:9  Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
Luke Swahili 4:10  kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
Luke Swahili 4:11  na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
Luke Swahili 4:12  Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
Luke Swahili 4:13  Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
Luke Swahili 4:14  Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
Luke Swahili 4:15  Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
Luke Swahili 4:16  Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
Luke Swahili 4:17  Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
Luke Swahili 4:18  "Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
Luke Swahili 4:20  Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
Luke Swahili 4:21  Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
Luke Swahili 4:22  Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
Luke Swahili 4:23  Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
Luke Swahili 4:24  Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
Luke Swahili 4:25  Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
Luke Swahili 4:26  Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
Luke Swahili 4:27  Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
Luke Swahili 4:28  Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
Luke Swahili 4:29  Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
Luke Swahili 4:31  Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
Luke Swahili 4:32  Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
Luke Swahili 4:33  Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
Luke Swahili 4:34  "We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
Luke Swahili 4:35  Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
Luke Swahili 4:36  Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
Luke Swahili 4:37  Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
Luke Swahili 4:38  Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
Luke Swahili 4:39  Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
Luke Swahili 4:40  Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
Luke Swahili 4:41  Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
Luke Swahili 4:42  Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
Luke Swahili 4:43  Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."