Site uses cookies to provide basic functionality.

OK
MATTHEW
Prev Up Next Toggle notes
Chapter 24
Matt Swahili 24:1  Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.
Matt Swahili 24:2  Yesu akawaambia, "Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
Matt Swahili 24:3  Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, "Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?"
Matt Swahili 24:4  Yesu akawajibu, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
Matt Swahili 24:5  Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye Kristo, nao watawapotosha watu wengi.
Matt Swahili 24:6  Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
Matt Swahili 24:7  Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.
Matt Swahili 24:8  Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
Matt Swahili 24:9  "Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.
Matt Swahili 24:10  Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.
Matt Swahili 24:11  Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.
Matt Swahili 24:12  Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.
Matt Swahili 24:14  Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
Matt Swahili 24:15  "Basi, mtakapoona Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),
Matt Swahili 24:17  Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.
Matt Swahili 24:19  Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
Matt Swahili 24:20  Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!
Matt Swahili 24:21  Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.
Matt Swahili 24:22  Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
Matt Swahili 24:23  "Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: Kristo yuko hapa au Yuko pale, msimsadiki.
Matt Swahili 24:24  Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.
Matt Swahili 24:26  Basi, wakiwaambieni, Tazameni, yuko jangwani, msiende huko; au, Tazameni, amejificha ndani, msisadiki;
Matt Swahili 24:27  maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
Matt Swahili 24:29  "Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
Matt Swahili 24:30  Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.
Matt Swahili 24:31  Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.
Matt Swahili 24:32  "Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
Matt Swahili 24:33  Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.
Matt Swahili 24:34  Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
Matt Swahili 24:35  Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Matt Swahili 24:36  "Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.
Matt Swahili 24:37  Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
Matt Swahili 24:38  Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.
Matt Swahili 24:39  Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.
Matt Swahili 24:40  Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
Matt Swahili 24:41  Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
Matt Swahili 24:42  Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.
Matt Swahili 24:43  Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
Matt Swahili 24:44  Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
Matt Swahili 24:45  Yesu akaendelea kusema, "Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?
Matt Swahili 24:46  Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
Matt Swahili 24:47  Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
Matt Swahili 24:48  Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: Bwana wangu anakawia kurudi,
Matt Swahili 24:49  kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
Matt Swahili 24:50  bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
Matt Swahili 24:51  Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.